Jinsi ya kujifunza na utaratibu wake

Stashahada (Diploma) ya masomo ya Sharia katika Afrika Academy inafundishwa katika mfumo wa kozi, ambapo kozi zinafundishwa mfululizo, ambapo wanafunzi husoma somo moja hadi wakamilishe pamoja na lulifanyia mtihani, na kisha kuendelea na somo linalofuata.

kozi hutolewa kwa njia ya

Video za mihadhara katika chaneli ya Africa TV

Mihadhara ya sauti (mp3)

Vitabu (pdf)

Matangazo ya moja kwa moja kwenye YouTube

Muda wa masomo katika programu ya diploma (stashahada):
  • Programu ya Diploma (stashahada) katika masomo ya Sharia katika Afrika Academy ina mihula miwili,kila muhula huchukua miezi 6, ambayo inakusanya masomo, mitihani pamoja na likizo. Na mpango programu nzima ya diploma hukamilika katika miezi 12. Na hapa kuna likizo fupi baina ya mihula miwili.
Mitihani na matokeo:
  • Mitihani :

Ni mitihani ambayo huwa mwishoni mwa kozi kwa lengo la kupima ufahamu wa wanafunzi na kutathmini uwezo wao, na ni mitihani ya lazima kwa kila kozi, ambayo muda wa kufanyika kwake huwa ni siku tatu.

  • Mitihani ya marudio:

Ni mitihani ya  kufidia/marudio kwa wanafunzi ambao hawakufikia daraja la kufaulu katika mitihani ya msingi au hawakufaulu mitihani ya msingi.

Mitihani yote hii hutolewa kwa mara moja mwisho wa muhula – mtihani wa kufidia/marudio kwa kila kozi – na muda wake ni siku kumi.

Alama na namna ya kuhesabu matokeo
  • Jumla ya alama kwa kila kozi ni 100

  • Alama ya kufaulu katika mitihani ya mwanzo au mitihani ya kufidia/marudio ni 50 au zaidi

  • Mwanafunzi hahesabiwi kuwa amefaulu katika muhula isipokuwa atakapomaliza kozi zake zote.
  • Baada ya kumaliza kila kozi, mwanafunzi ataonyeshwa alama zake alizozipata.
Cheti

Kwa kupata alama za ufaulu katika mihula miwili, mwanafunzi ana haki ya kupata cheti cha kidigitali kinachotolewa na Academy, ambacho anaweza kukisoma na kupakua kutoka ndani ya akaunti yake kwenye jukwaa.

Programu shirikishi
  • Katika kipindi chote cha masomo, kuna programu shirikishi na mashindano yenye mwenendo wa kielimu na mengine yana lengo la kumtengenezea mwanafunzi mazingira ya kuhamasisha, kuburudisha na kuwasaidia kuendelea na mchakato wa elimu na sio kuikatiza.
  • Programu hizi zote ziko kwenye vikundi shirikishi na vya kujifunza kwenye tovuti ya mawasiliano (mtandao wa kijamii) uliochaguliwa kwa ajili ya kujifunza.
×