Africa Academy

Jukwaa la Kiafrika la mtandaoni la kufundisha Elimu ya Kisheria bure kabisa.

Video ya namna ya kujisajili katika Academy

Africa Academy ni akademi ya mtandao/kielektroniki inayotoa programu ya elimu kwa lengo la kuzisaidia jamii za Kiafrika kuwa na ufahamu sahihi wa Uislamu kwa kuzingatia ushahidi wa Qur’ani Tukufu na Sunnah za Mtume, kwa kutumia mtandao wa intaneti, mitandao ya kijamii. na luninga za chaneli za Afrika TV. Akademia hii inatokana na kada mashuhuri ya wanazuoni na mashekhe mashuhuri wa Ahlu Sunnah Wal-Jama’ah wanaozungumza lugha za Kiafrika.

Programu za Akademi

Mpango wa masomo

Akademi inategemea mfumo wa masomo wa masafa (kupitia mtandao) , ambapo mwanafunzi anachagua njia ya kusomea ambayo inaendana nae zaidi miongoni mwa njia tofauti zinazopatikana.

Pakua faili la mwongozo wa mwanafunzi kufahamu mpango kamili wa masomo katika jukwaa

Habari

Tunapenda kuwatangazia kuwa usajili wa Academy utafungwa siku ….

Tunawapa bishara kwamba usajili katika programu ya Stashahada

kozi hutolewa kwa njia ya

Video za mihadhara katika chaneli ya Africa TV

Mihadhara ya sauti (mp3)

Vitabu (pdf)

Matangazo ya moja kwa moja kwenye YouTube

Masomo yanayofundishwa

Jopo la walimu (Walimu wa kitivo)

Sheikh Ally Nassor

Sheikh Hassan Muhammadyn

Sheikh Shamsi Elmi

Sheikh Muharam Mwaita

Sheikh Salim Qahtwaan

Sheikh Shahid Mohammed

Programu ya Stashahada ya Elimu ya Kisheria

Programu nzito ya kielimu ya elimu za Sharia kwa muda wa mwaka mmoja, ambapo yanakuwa masomo kwa mfumo wa makundi, ambapo makundi ya kimasomo huwa kwa vipindi maalum katika mwaka na kutangazwa kwa njia mbalimbali za mawasiliano na luninga za chaneli za Afrika TV, na usajili wake hufunguliwa kwa muda wa kutosha kabla ya kuanza. Na programu ya stashahada huwa na mihula miwili ambayo mwanafunzi anasoma masomo sita katika kila muhula, na baada ya mwanafunzi kufaulu mitihani ya mwisho kwa mihula miwili, anapata stashahada ya elimu ya Sharia kutoka Africa Academy.

Semina fupi za wazi

Kozi fupi za Sharia zinazozungumzia mada moja au zaidi katika yale ambayo Muislamu hatakiwi kutokuyajuamiongoni mwa elimu za kisheria. Usajili wa kozi hizo huwa wazi siku zote, ili mwanafunzi aweze kujiunga na kozi hiyo wakati wowote anaotaka na kusoma kwa wakati unaomfaa na kwa kiasi kinachomfaa, na baada ya kumaliza kozi na kufaulu mtihani wake mwanafunzi anapata cheti cha kuhitimu kozi hiyo.

Takwimu za Akademi

Idadi ya wanafunzi waliosajiliwa

20000

Idadi ya wanafunzi waliohitimu

20000

Wanaofwata mitandao ya kijamii

20000

Habari za hivi karibuni
×